HEADER

Jumatano, 31 Julai 2013

APOSTE GIDEON MUTALEMWA ALIYOYAFANYA MAFINGA IRINGA WIKI YA JANA NA KUSABABISHA KUPATA MUALIKO MWINGINE MKOANI HUMO

Mungu bado anazidi kumtumia mtumishi wa Mungu Mtume Gideon Mutalemwa wa anayeabudu katika kanisa la Yesu Kristo la Huduma ya Maombezi na Uponyaji lililochini ya Nabii Flora hapa jijini Dar es Salaam.

Wiki iliyopita alikuwa katika mkoa Iringa eneo la Mafinga kwa kazi ya Mungu katika mkutano wa nje ulioandaliwa na kanisa la Jerusalem Spiritual Transformation lililoko Lumwago Mafinga Iringa mjini siku ya tarehe 24 hadi 28/07/2013.Na sasa ameingia jijini Dar es Salaam kwa kazi ya Mungu.

Siku ya tarehe 8.2013 anategemea kurudi tena katika mkoa wa Iringa ambapo amepata mwaliko na  Mchungaji Ambakisye wa kuhudumu katika kanisa la HOPE FOR ALL NATION CHURCH MAFINGA IRINGA TANZANIA

Mkutano huo ni mkutani wa nje utakaoanza siku ya tarehe 06.08.2013, eneo: Mafinga Mjini uwanja wa kanisa kuanzaia saa9:00 Alasiri – 12: 00 Jioni.

Kumbuka Apostle Gideon ni mwimbaji wa nyimbo za injili Tanzania na pia anafanya kazi ya kuhubiri katika mikutano mbalimbali, Na sasa hivi ameachia albamu yake ya Sambamba na Yesu ambayo ilifanyiwa shooting upya kwa kiwango cha juu sana.

Unaweza kuwasiliana naye kwa simu: +255 719 697252 au tembelea katika blogu yake ya www.apostlegideon.blogspot.com



Apostle Gideon Mutalemwa akihudumu katika kanisa la Yesu Kristo la Huduma ya Maombezi na Uponyaji la Nabii Flora Peter lililoko Mbezi Salasala jijini Dar es Salaama. Unaweza kutembelea blogu ya kanisa hili www.nabiiflora.blogspot.com au ingia katika facebook yake kwa jina la Nabii Flora Peter.

APOSTLE GIDEON MUTALEMWA AKIWA MKOA WA IRINGA WIKI YA JANA

Mtume Gideon Mutalemwa akiwasha moto Mafinga
 Kwaya ikimtukuza Mungu kwa njia ya uimbaji

Mtume Gideon Mutalemwa akihubiri kabla kuanza kazi ya kumuimbia Mungu
Kwaya ikifnaya kazi ya Mungu wakati wa mkutano

Kazi ya Mungu ikifanywa na Apostle Gideon Mutalemwa
 Wachungaji na Maskofu wakisikiliza Neno na kusoma Neno la Mungu

Haya sasa, mtumishishi wa Mungu akitumika...kurudisha watu kwa Yesu Kristo
Watu full kujiachia kwa Yesu Kristo

Mafinga ikiwashwa moto na Mtumishi wa Mungu Apostle Gideon Mutalemwa.
Watu walkiselebuka na Yesu wakati mtume Gideon akifanya mambo ya Yesu

mzee wa Sambamba na Yesu, Mtume Gideon Mutalemwa akienda sambamba na akina Kamwene na Mapembeleo mjini Mafinga

Kama wewe hupendi kumuimbia Mungu, Mtume Gideon Mutalemwa atamwimbia, kama unavyoona akifanya mambo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...