HEADER

Ijumaa, 12 Julai 2013

NEEMA GASPA KUMILIKI BLOGU YAKE YA KIKRISTO

Neema Gaspa ni mwimbaji wa nyimbo za injili, siku ya Jumatatu ameweza kufungua blogu yake mpya inayoenda kwa link hii: www.neemagaspaa.blogspot.com. Katika blog hii utapata kujua mengi kuhusu yeye na huduma yake.

Neema Gaspa akiwa katika ofisi ya Rumafrica Sinza Afrikasana

Blogu hii itakuwa inaweka habari za Mungu kutoka madhehebu mbalimbali nchini Tanzania na nje ya Tanzania. Lengo kuu ni kumtangaza huyu Yesu Kristo kwa njia ya mitandao.

Blogu hii imetengenezwa na RUMAFRICA. Rumafrica wanajishughulisha a shughuli za Graphics, shooting, kutengeneza blogs, websites, na kupiga still picture. Unaweza kuwasiliana nao kwa simu +255 715 85 15 23 au tembelea www.rumaafrica.blogspot.com au www.rumaafricajobs.blogspot.com


Neema Gaspa kwa sasa anajiandaa na kuzindua albamu yake inayoenda kwa jina la SHUJAA itakayofanyika katika ukumbi wa Ubungo Plaza siku ya tarehe 01.09.2013 kuanzia saa 7:00 mchana na kuendelea. Kiingilio ni Tsh. 10,000 kwa VIP, watoto ni Tsh. 2,000 na viti vya kawaida ni Tsh. 5,000.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...