HEADER

Jumatatu, 8 Julai 2013

VIJANA WASHEREHEKEA SABA SABA HOSPITALI YA AMANA KUTOA MISAADA NA MAOMBI


Kundi la vijana kutoka kanisa la Living water Kitunda jijini Dar es salaam, hapo jana walisherehekea sikukuu ya sabasaba kwakwenda kuwatembelea wagonjwa katika hospitali ya Amana iliyopo wilayani Ilala jijini Dar es salaam kwakuwapa misaada mbalimbali pamoja na kuwafanyia maombi.

Katika mahojiano na GK mtumishi Gasper Madumla kutoka knisa hilo ameelezea vitu mbalimbali walivyotoa kwa wagonjwa na hali ilivyokuwa "Tulienda Amana hospital kwa ajili ya maombezi na misaada kwa wagonjwa hususani hodi ya wazazi. tulipangiwa wodi ya wazazi kuanzia saa kumi hadi saa kumi na mbili jioni. tuliwapelekea vitu kama dawa za matibabu,Vifaa tiba mfano nyembe,groves,tishu,sindano,pamba,pia sabuni,pia tulifanya maombi kwa wakina mama waliojifungua na hata wale waliokuwa hawana uchungu nao wote wakapokea uponyaji mkuu.Pia tulikuwa na vifaa tiba vingine kama Derto,pempasi, Tulianza kwa kufunga na kuomba wiki nzima kabla ya kwenda hospitalin ili msaada huo uwe na uponyaji ndani yake niliendesha maombi ya nguvu kabla tu hatujafika hospitali kwa kuvitakasa vifaa hivyo kwa yeyote yule mwenye kuvitumia vimponye bila kujali dini au itikadi yake ya dhehebu" amesema mtumishi Madumla

Aidha mtumishi huyo ameongeza kuwa"Na baada tu ya kuwasili hospitalini hapo,tulipokelewa vizuri sana kisha tukaoneshwa wordi ya wazazi mahali ambapo wakina mama mara nyingi wajifunguapo hupoteza watoto wao,au mara nyingi hujifungua kwa taabu sana,hivyo tulipopelekwa katika wordi hiyo,tukaanza kazi ya kuwapa misaada na kufanya maombezi rasmi ili isije ikajitokeza hali ya kupoteza mtoto na hata uchungu uwe wa kawaida kwamba Bwana afanye wepesi katika hali yao ya kujifungua. Kwa sababu ilikuwa ni wordi ya wazazi,walipendelea waingie wanawake kwa huduma ya kiroho maana nilikuja nao wanawake ambao ni watumishi wa Mungu,nao wakaichapa kazi vizuri ,hakika wote walibarikiwa. Ilipofika saa kumi na mbili tulikuwa tumemaliza na kuanza kurejea nyumbani.




 Source: GK

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...