HEADER

Jumatano, 10 Julai 2013

USIKOSE KATIKA UZINDUZI WA ALBAMU YA SHUJAA YA NEEMA GASPA-UBUNGO PLAZA

Umehudhuria matamasha mengi lakini hili si la kukosa kwani kuna kitu Mungu anaenda kufanya juu ya maisha yako katika siku hii ya uzinduzi wa albamu ya mwaimbaji wa kimataifa wa nyimbo za injili Tanzani Neema anayeenda kuzindua albamu yake ya kwanza inayoenda kwa jina la SHUJAA. Utakuwa unajiliuliza ni nani Shujaaa..majibu anayo Neema Gaspa.

Neema Gaspa

Mungu anamtumia sana huyu mtumishi wa Mungu kwa njia ya uimbaji.  Neema Gaspa anatumia ujana wake kwa kazi ya Mungu, na huu ni moyo wa kipekee sana. Neema Gaspa baada ya kuona watu wengi wanauhitaji na kiu ya kutaka kufaidika na karama yake ya uimbaji, sasa ameamua kuzindua albamu yake ili karama yake wapate kuisikia na mwisho wa siku ni kumpa Mungu utukufu kwa maana YEYE anastahili.

Tunachokuomba ni wewe kufika katika eneo la tamasha Ubungo Plaza ili kumuunga mkono mtumishi wa Mungu. Umefika wakati wa kuwa busy sana kumtafuta Mungu. Unaposikia jambo fulani linafanyika kwa utukufu wa Mungu unatakiwa kuamka na kukimbia kumsifu Mungu wetu. Naye Mungu atajisikia furaha sana kuona mtoto wake ameacha kazi zake na kuungana na watu wanamsifu.

Sasa usikose kabisa kufika katika uzinduzi huu. Ikiwezekana mtaarifua na rafiki yako ili aweze kupokea muujiza wake kwa njia ya uimbaji.

Mgeni Rasmi katika uzinduzi huu ni Mheshimiwa Samweli Sitta  aliyekuwa Spika wa Bunge katika Jamhuri ya Tanzania
Mh. Samweli Sitta

Uzinduzi utafanyika katika jengo la kifahari la UBUNGO PLAZA, kwani hata MUNGU wetu wa kifahari sana na wa thamani sana ndio maana tumeona lazima asifiwe katika eneo linaloendana  na uthamani wake
Jengo la Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam

Kutakuwa na waimbaji wengi sana wa kimataifa kutoka nchini, baadhi yao ni kama:

AMBWENE MWASONGWE

BAHATI BUKUKU


EDSON MWASABWITE
 EVELYN MSOMA


MADAM RUTI

MARTH MWAIPAJA

MAXIMILLANI MWANAMAPINDUZI
 ENOCK JONASI

KIINGILIO KITAKUWA KAMA IFUATAVYO


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...