HEADER

Jumatatu, 8 Julai 2013

HAPPY BIRTDAY NABII FLORA PETER KWA KUTIMIZA MIAKA 29 LEO TAREHE 07.07.2013


Jumapili ya leo ilikuwa ni ya kipekee sana kwa waumini wa kanisa la Yesu Kristo la Huduma ya Maombezi na Uponyaji Mbezi Salasala hapa jijini Dar es Salaam. Nabii Flora amezaliwa siku ya leo akiwa kanisani. Wapo watu wengi wanazaliwa siku ya leo wakiwa katika mabaa na sehemu mbaya, lakini tunamshukuru Mungu kwa kumuwezesha Nabii Flora kuzaliwa siku ya leo akiwa kanisani na watu wa Mungu.

Kwa kweli Mungu ni mwema kwa kumtimizia miaka 29 Nabii Flora Marco. Mungu amekuwa mwema sana katika huduma yake ya kurudisha watu kwa Mungu. Watu wamebarikiwa sana na siku ya leo. Kanisani kulifanyika tamasha kubwa sana kwaajili ya kumpongeza Nabii Flora kutimiza miaka yake 29. Nabii Flora aliwashukuru sana waumini wa kanisa hilo kwani amesema wamefanyika kuwa kama familia yake.

Nabii alionekana kuhuzunika pale tu alipoweza kutoa historia ya maisha yake kabla na baada ya kuwapoteza wazazi wake wote wawili. Historia hii iliwagusa sana watu wengi waliofika na kuhudhuri siku ya kumpongeza Nabii Flora. Ni mengi Nabii Flora amepitia katika huduma yake ikiwa ni pamoja na kupata vipingamizi vingi katika kazi ya Mungu. Alisema ilifika kipindi akawa anakula na kunya maji ya nazi kutokana na kutokuwa na chakula ndani ya nyumba yake.

Nabii Flora alimshukuru sana Mchungaji Ansilla kwa msaada mkubwa sana katika maish yake, na alisema anakumbuka birthday yake Nabii Flora alifanyiwa na mchungaji huyu. Pia alimshukuru Octavian ambaye alikuwa akimsaidia sana katika kupiga picha wakati akihubiri kwa kutumia kamera yake na bila malipo, alimshukuru sana Mchungaji Komba kwani amekuwa bega kwa bega tangia wameanza huduma hii, alimshukukru Mchungaji Jury kwa kukubali kufanaya naye kazi ya Mungu kwani mara ya kwanza wamekutana Nabii Flora alimwambia ninaona una huduma ya uchungaji ndani yako lakini Mchungaji Jury hakutambua hilo na sasa ni Mchungaji katika kanisa la Nabii Flora. Aliwashukuru wazee wa kanisa kwa kazi wanafanya katika nyumba ya Mungu. Alimshukuru sana katibu wa kanisa kwa wametoka naye mbali sana katika kazi ya Mungu. Alimshukuru sana sana Salma ambaye ni mtu wa kwanza kufanya naye kazi ya Mungu, Salma alikuwa akimsaidia Nabii Flora kumpeleka saloon, kumsafirisha kipindi hana gari, kumtia moyo asonge mbele na mambo mengi mengi sana.


Kikundi cha vijana kikielekea madbahuni kwaajili ya kufungua Shampeni




 Wakiwa wamevua kofia kwa kumheshimu Nabii Flora baada ya kufika madhabahuni kwa zoezi la kufungu shampeni
 Kilifika kipindi cha kucheza na kufurahi
 
Nabii Flora akifanya Maombezi kwa kufungua shughuli ya leo
Wakisujudu wakati Nabii Flora akifanya maombi

Nabii Flora katika maombi


 Nasbii Flora akisubiria nini kinafuata baada ya maombi
 Mmoja wa watumishi wa Mungu akimpa glasi kwajili ya shampeni
 Watumishi wa Mungu wakifungua Shampeni







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...