Atakulinda Yeye wala hata sinzia, hata kubali mguu wako
usogezwe wachawi wasogeze mguu wako, kifo kisogeze mguu wako, mateso yasogeze
mguu wako yaani hata kubali atakulinda pokea, anaema sinta kuacha jua halite
kupiga mchana wala usiku. Nataka ulindwe mama nyumba yako izungushiwe kuta za
moto wanapotuma vingwendu, roboti zitashindwa kufanya kazi.

Mchungaji Komba

Mchungaji Komba
Naona mamlaka zinatembea anasema duniani ni sehemu yangu ya
kuweka mguu wangu, naona miguu ya Yesu inatembea inakausha Ukimwi, Kansa,
uvimbe, inaondoa magonjwa, utasa, mapepo inamamlaka ikikanyaga inafuta mateso.
Nasema na watu wanaonitazama kwenye youtube maana upo mguu yapo mamlaka ya Yesu
yameshuka leo.


Anasema duniani ni sehemu yangu ya kukanyaga lakini mbinguni
ni sehemu ya kiti change cha enzi, nataka Bwana asimame leo, naona mamlaka
inatembea naona uweza wa Yesu naona miguu ya Yesu mama anakanyaga magonjwa,
umasikini, Ukimwi, mapepo, utasa, mateso chini ya kitovu nakwambia achia
utaweka mamlaka ya Yesu. Unamaruhani , unamizimu, unamajini mahaba ipo mamlaka
inakanyaga, sauti ya Yesu inakuita fanya hima ufike haraka anakuita wewe
unayenitazama kwenye yuotube, unayenisoma kwenye facebook na blogu sauti ya
Bwana inakuita asubuhi ya leo.


Anakuita wewe muombaji ulikuwa unaweza kuomba lakini sasa
hivi unapiga miayo tu sauti ya Bwana inakuita baba, mama, kijana usifanye moyo
wako kuwa mgumu sauti ya Bwana inakuita ameshuka mwenye mamlaka ipo sauti ya
Mungu inawaita watanzania, watu mbalimbai wanaonitazama kwenye youtube na
kunisoma kwenye blogu na facebook yupo Yesu anakuita leo.


Anasema geuke
unapokwenda unaenda kuangamia hiyo biashara waliyo kushirikisha nakwambia sio
sahihi unakwenda kukamatwa utaishia sero nakwambia acha biashara hiyo wewe
unayenitazama kwenye youtube, unayeshirikishwa biashara na rafiki zako wa tatu
mmoja mfupi mweusi anamwanya chini mwingine mrefu amenyoa panki tena mweupe
nasema hiyo biashara waliyo kushirikisha unakwenda kukamatwa utaishia polisi.
Usikiapo sauti hii nasema geuka ipo Baraka zipo kazi nyingi nyingi mbele za
Bwana utafanya kazi zako utabarikiwa.


Hakika ninasika sauti ya Bwana inakuita, Mtanzania , mwana
Dar es salaam kwamba njoo uitende kazi yake wewe unayekaa vijiweni hasubuhi
mpaka jioni wewe unafuata tu kivuli sauti ya Yesu inakuita leo, inakuita uje
utende kazi yake.

Usikiapo sauti hii geuka wakati wa neema ni sasa usije ukakawia ukachelewa ukakuta neema kwako imeondolewa, Yesu anakuita asubuhi ya leo amesema duniani ni sehemu ya kuweka miguu yake mbinguni ni nsehemu ya kiti chake cha enzi. Anataka akanyage mateso kwako maana ipo mamlaka kwake akikanyaga anaondoa taabu zako zote.


Usikiapo sauti hii geuka wakati wa neema ni sasa usije ukakawia ukachelewa ukakuta neema kwako imeondolewa, Yesu anakuita asubuhi ya leo amesema duniani ni sehemu ya kuweka miguu yake mbinguni ni nsehemu ya kiti chake cha enzi. Anataka akanyage mateso kwako maana ipo mamlaka kwake akikanyaga anaondoa taabu zako zote.

Somo linatoka katika kitabu cha Mwanzo 28:16-22
Mwanzo 28:16-22
Nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa Baba yangu ndipo na wewe Mungu utakapo
kuwa Mungu wangu. Na jiwe hili ninalo lisimamisha hapa nitaijenga nyumba yako
Bwana, na kwa kila kitu kitakapopita mikononi mwangu nitakutolea wewe Mungu.
Yakobo alipoamka asubuhi na mapema akalitwaa lilie jiwe alilokuwa ameliweka juu
ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo na kumimina mafuta juu yake akapaita
mahali pale jina lake Betheli, lakini ule mti baada ya hapo ulikuwa unaitwa
Luzu. Yaani Luzu ni mji wenye ukame
Mchungaji Komba akitafsiri lugha ambayo nabii Flora alikuwa akinena

Mchungaji Komba akitafsiri lugha ambayo nabii Flora alikuwa akinena
Yamkini wewe unaitwa mtu ambaye awezi kuwa na gari,
nazungumza na mtu ambaye leo anahitaji kubadilika, wewe unayetaka kubadilika
kutoka katika hali ya ukame na huitwe mtu mwenye Baraka, uliye nawiri. Maisha
yako yabadilike ulikuwa unakunywa chai ya rangi unywe chai ya maziwa, ulikuwa
unakula mlo mmoja ule milo mi tatu utatoka katika hali ya kuitwa Luzu na utaitwa
Betheli.


Bwana akamwambia msipande mazao katika mji wa Luzu, mji wa Luzu ni mji
wenye jiwe la chumvi hauoteshi chochote. Kwa hiyo sasa naamuru watu hawa
wasipande chochote katika mji wa Luzu; yaani mti wa Luzu
unajikutaumetoa sana sadaka huoni kinachoendelea ni mji wa Luzu umepanda,
umetoa fungu la kumi lakini bado umefilisika, ulitoa Luzu sasa njoo weka hapa
Betheli. Yaani jiwe la chumvi hauoteshi chochote hata maji ukiyanywa hayana
ladha.

Dada kichaa aliyeletwa kwa maombezi


Dada kichaa aliyeletwa kwa maombezi

Nendeni Betheli mkapande kila aina yam mea na kila aina ya nafaka na kila
mti wa matunda, pandeni humo katika mji wa Betheli kwa sababu udongo wake,
udong wa baraka. Hii ni huduma ya Baraka hata kama umeachwa na mume,
mume atwrudi kwa mke wake wan ndoa panda
miguuni kwa Nabii maana kuna udogo mzuri. Yaani katika kanisa la Yesu ipo
miujiza watu wanapona Ukimwi, vipofu wanaona, viwete wananyooka miguu, vilema
wanafunguka panda hapa katika mji wa Betheli, umekataliwa hujazaa umetolewa
kizazi panda mbegu zako hapa hakika utazivuna.


Yakobo akaamka katika usingizi wake akasema kweli bwana yupo mahali hapa, wala mimi
sikujua kama bwana yupo. Naye akaogopa
akasema kweli Mungu yupo mahali hapa wala mimi sikujua, na hapa ndipo lango loa mbinguni. Yamkini
wewe umekuja Mtanzania, unayenitazama kwenye youtube, unayenisoma kwenye blogu
na facebook. Yakobo alishangaa akasema mbona
hapa panatisha kama nini akasema bilashaka hapa ni nyumba ya Mungu,
miujiza watu wanapona magonjwa mbali mbali, akisema hewa geuka inageuka,
akisema miti sujudu miti inasujudu maana hapa panatisha kama nini.


Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe lililokuwa
chini ya kichwa chake akalisimamisha kama nguzo na kumimina mafuta juu yake
akapaita mahali pale jina lake Betheli. Nami nakutamkia Baraka siku ya
leo ya kureje fedha na shekel, nakutamkia Baraka hata kama ulitamkia laana na
mama mkwe, mama yako, shangazi naifuta laana nakutamkia baraka.


Yakobo akaweka nadhiri akasema Mungu ikiwa atakuwa pamoja nami,
akinilinda katika safari ninayo iyendea na kunipa chakula nile, na mavazi
nikavaa na nitarudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu ndipo Bwana atakuwa Mungu
wangu na jiwe hili ninalo lisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu hapa,
na katika kila utakalo nipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi.

Laana zilimpata baba yetu wa imani ndipo watoto wake wa
kwanza wa kiume walilala na wake zake, ukitoa nadhiri usipo hiyondoa na ndo
maana mimi nilimwambia Mungu kama utanifanikisha nimalize jengo Salasala
nitakutolea ng’ombe ili watoto wangu wasije wakafanya laana wao kwa wao. Ili
laana niifute nilichinja ng’ombe wa tatu,
watu hawakujua nilitoa nadhiri kwa Mungu nikamwambia Mungu kama utanifanikisha
nikalimaliza jengo hili kwa miezi mi tatu nitakutolea ng’ombe.


Kumbe nadhiri ni kitu sio cha mchezo ukisema Nabii nitatoa
fungu la kumi toa, chagueni sasa leo kama utakuwa Luzu ama utakuwa Betheli.
Yaani Luzu ni nchi isiyo kubali zao lolote, chakueni wa baba na wa mama unapenda kukaa nchi gani na leo ni siku ya
tatu ya uumbaji ambayo Mungu aliumba, Mungu nataka leo uwatendee watu hawa.
SIKILIZA USHUHUDA WA KIZITO
SIKILIZA USHUHUDA WA KIZITO
Kwa jina naitwa Kizito nilikua hapa nikiwa na
matatizo yangu ma nne nikaa na Nabii nikamweleza matatizo yangu, akasema
nichague tatizo langu moja ili niweze kuliombea basi nikamwambia naomba kazi.
Nilikuwa naimesha tumia juhudi zngu za mwili na elimu yangu lakini
haikuwezekana, nilikuwa nimeshapeleka application za kazi karibu hamsini lakini
sikujibiwa hata moja.
Baada ya kuja hapa Nabii akaniambia naona ukuta mkubwa
sana juu yako na sasa naingia kwenye maombi kuuvunja huu ukuta, na kweli siku
ambayo alikuwa ameniahidi nitapata kazi, siku moja kabla nikapokea email kwamba
nipo tayari kufanya kazi. Na siku ambayo Nabii aliniambia ndiyo nitapata kazi
nilipigiwa simu niende nikafanye interview, kwa kweli hapa mmefika ndo mahali
pake.



Yakobo akaweka nadhiri akasema Mungu ikiwa atakuwa pamoja nami,
akinilinda katika safari ninayo iyendea na kunipa chakula nile, na mavazi
nikavaa na nitarudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu ndipo Bwana atakuwa Mungu
wangu na jiwe hili ninalo lisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu hapa,
na katika kila utakalo nipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi.

Tutakuwa na wageni mbali mbali siku ya jumapili watatembelea katika kituo hiki, kutakuwa na
ibada ya ajabu sana kwa kweli ni ya kuufungua mwezi na nikwambie mwezi huu
unalenga nini na nikwambie haki zako za mwezi wa sita. Nataka nikwambie leo ni
tarehe 29 tunaelekea kufunga mwezi Abuu, kesho tarehe 30 tunamalizia Ijumaa,
Jumamosi tarehe 1 na Jumapili itakuwa tarehe 2, itakuwa ni ibadayetu ya mwanzo
wa mwezi ambayo tutapaka mafuta.


Kila ilipofika mwisho
wa mwezi Nabii Eliya alipita kwa mwanamke mshumemo, ataalipokuwa mapambavuko
aliingia katika ile nyumba ya mwana mke wa cheo, nitakupa habari za mwana mke
mshumemo walipokuwa wakiingia nyumbani kwa mtumishi wa Mungu alipanda kitu gani.
Mwanzo wa mwezi, mwisho wa mwezi ni kitu gani kinatokea.
Ujapozimwa nyota hapa inang’aa, hata kama wameizima
wameikalia, wameifunika hapa tunaifungua kwa jina la yesu.
SHUHUDA
DADA ALIYEKUWA
ANATAFUTA KAZI SASA AMEPATA


Bwana Yesu asifiwe, kwa jina naitwa Mwajabu; asubuhi mimi
nilikuja nikamwambia Nabii kwa nini mimi sipati kazi, Nabii akaniombea
akaniambia kuanzia sasa hivi naamuru upate kazi, narudi kukaa kwenye kiti
napigiwa simu naambiwa kunakazi kwenye
sekondari moja ambayo nili applay nimeambiwa
nikaanze kazi.
KIJANA ALIYEKUWA
AMEPOTEA SASA AMERUDI NYUMBANI

Pia nilikuja hapa na
mama mwenye nyumba wangu akamwambia Nabii kijana wake amepotea Nabii akamwambia
ataonekana kweli baada ya maombi siku
hiyo tupo sokoni na dada yake tukamuona, ndo akarudi nyumbani moja kwa moja.
DADA ALIYEKUWA ANAOMA
KALI SASA AMEPOA

Kwa jina naitwa Beatrice Wiliamu; mimi namshukuru Mungu
wa madhabahu hii ameniponya, ni juzi tu
nilkuwa naumwa sana yaa kiukweli hali yangu ilikuwa mbaya mno kichwa kinauma
homa kali natetemeka. Sasa wakati naumwa
na mbwa wangu na yeye alikuwa anaumwa sana, basi mdogo wangu akampigia
Nabii akamwambia aniombee, baada ya Nabii kuniombea nikajisikia nafuu lakini
baada ya kuamka asubuhi nikajikua mzima, yaani ile vita ilikuwa ni kubwa mbwa
wangu yeye alikufa.
MTOTO ALIYEKUNYWA
SUMU AMEPONA
Kwa jina naitwa Anastanzia Elius; nashukuru madhabahu ya
Nabii Flora yanazidi kuniokoa tu maana kila niachohitaji nikija hapa nikiomba Mungu ananitendea. Mimi
juzi nilipigiwa simu nikaambiwa mdogo wangu anaumwa sana aikuwa amekunywa sumu,
lakini baada ya maombi amepona kwa kweli namshukuru Mungu.
MAMA ALIYEKUWA NA
UGOMVI NYUMBANI KWAKE SASA MAELEWANO YAMERUDI

Kwa jina naitwa Johanitha; mimi nimeanza maombi hapa mwezi
wa pili, nilikuwa ninavita kwenye familia yangu mpaka nafika hatua nakata tama,
lakini baada ya maombi namshukuru Mungu amenirudishia amani ndani ya nyumba
yangu, mume wangu amerudi na mgogoro na mama mkwe wangu umeisha namshukuru sana
Mungu.
MTOTO ALIYEKUWA
ANAUMWA SASA AMEPONA

Kwa jina naitwa Leah; mimi namshukuru Mungu kupitia madhabahu hii
kwa sababu wiki iliyopita mtoto wangu alikuwa naumwa sana, nimempeleka Hospitali lakini bado amepimwa hana ugonjwa,
nikampeleka tena Hospitali nyingine ndo akakutwa na almonia. Lakini mishipa
ikawa haionekani, nikampigia Nabii simu akamumbea mishipa ikaonekana na
akapatiwa huduma, nmshukuru Mungu mwanangu amepona mpaka leo.


Kanisa la Yesu Kristo la Huduma ya Maombezi na Uponyaji Mbezi Salasala Dar es Salaam Tanzania
Tembelea: www.nabiiflora.blogspot.com
www.rumaafrica.blogspot.com
Mob: +255 657442699


Kanisa la Yesu Kristo la Huduma ya Maombezi na Uponyaji Mbezi Salasala Dar es Salaam Tanzania
Tembelea: www.nabiiflora.blogspot.com
www.rumaafrica.blogspot.com
Mob: +255 657442699
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni