HEADER

Jumanne, 18 Juni 2013

RON KENOLY NA DON MOEN KUMPA TAFU ASKOFU KAKOBE NCHINI CANADA ALHAMIS HII



Mwimbaji nguli wa muziki wa injili duniani Ron Kenoly anatarajiwa kuwa mmoja wa waimbaji watakaoimba katika mkutano mkubwa wa injili wa kimataifa ulioandaliwa na askofu Zachary Kakobe ambao unatarajiwa kuanza alhamisi hii tarehe 20 hadi 23/6/2013 katika uwanja wa Rexall Centre Tennis katika jiji la Toronto nchini Canada.

Waimbaji ambao tayari wametajwa kuimba katika mkutano huo ambao umepewa jina la "Toronto Miracle Healing Crusade"ni pamoja na nguli mwingine Don Moen, kundi la wanandugu Krystaal, Martha Munniz na waimbaji wengineo, mkutano huo utakuwa wa kwanza kufanyika katika uwanja huo wa tennis huku pia askofu Kakobe kupitia huduma yake ya BZKIM inafanya kuwa muhubiri wa kwanza kutoka Tanzania na Afrika mashariki na kati kufanya mkutano mkubwa sehemu ya wazi kama ilivyo kwa watanzania kushuhudia wahubiri wakubwa wakija kuhubiri nchini.

Wiki iliyopita askofu Kakobe alikaririwa akiwatoa hofu waumini wake kutokana na madai ya kwamba amewatoroka na kuwaambia kwamba anakwenda kutimiza agizo la Mungu kuhubiri Canada katika mkutano mkubwa tena akitumia lugha ya Kiswahili. Kama hukusoma BONYEZA HAPA.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...